DOGO JANJA NA NDOTO YA KUTAJWA NA JARIDA LA FORBES


Dogo janja amesema anaweza kutajwa kwenye Jarida la Forbes under 30 iwapo mpango wake wa kuzindua brand kwa ajili ya watoto utafanikiwa
.
.

Dogo janja amedai kuwa mipango yake sio kuja na nguo kama ilivyozoeleka kwa wasanii wengi bali yeye mipango yake ni kuja na vifaa vya watoto vya michezo pamoja na magemu ambayo yatakuwa katika brand yake
.
.
. . "Brand ya Dogo janja itakuja lakini mimi sitakuja na Brand ya nguo, Nitakuja na vifaa vya watoto vya michezo vya Dogo janja nitakuja na magemu ya Dogo janja yani mimi biashara yangu itakuwa ina'deal na madogo dogo madogo janja" alisema @Dogojanjatz
.
.

Hata hivyo Janjaro ameweka wazi kwanini biashara yake ita'deal na watoto wadogo tu na si watu wazima
.
.
. "Biashara na mtoto, ujue ukifanya biashara na mtu mzima haitamuhusisha mtoto lakini ukifanya biashara na mtoto itamuhusisha mtu mzima" alieleza .
.

Dogojanja ameongeza kuwa yupo katika maandalizi ya kusafili na atakaporudi kwenye mwezi wa sita biashara hiyo itaingia sikoni rasmi

No comments

Powered by Blogger.