JOKATE MWEGELO - NILITEGEMEA KUTAJWA NA JARIDA LA FORBE


.
.
Baada ya kutajwa kwenye jarida la Forbes
kama mjasiriamali wa kutazama, Jokate
Mwegelo amefunguka kama aliwahi kuhisi
kama kuna siku atakuwepo kwenye list ya
Forbes .
.
Jokate amesema Kupitia kidoti wameweza
kushawishi vijana kujiajili, wameona fursa
na kuzitumia kwahiyo alitegemea kutajwa
kwenye Jarida la Forbes .
.
. "Pengine nilitegemea ningeweza siku moja
kutokea kwenye hiyo list kwasababu
ukiangalia kati ya vijana ambao wameweza
ku-inspire na ku- motivate vijana wenzao
kuweza kutafuta njia mbalimbali za
kujiingizia kipato kuwa wabunifu na fursa
ambazo zipo na jinsi gani ya kuzikamatia na
kujiongezea thamani. Lakini ukiachana na
hilo pia jinsi gani ya kuweza kujiajili
mwenyewe kwasababu sio kila mtu anaweza
kuajiliwa pengine wale wanaoweza kumaliza
chuo na hata wale ambao hawajafika chuo
lakini kuona tu fursa ambazo zipo na jinsi
gani ambavyo unaweza kuzikamatia nadhani
tumeweza kwa kiasi kikubwa kupitia brand ya
kidoti na kampeni mbalimbali kuweza kutoa
mwangaza huo na kushawishi vijana wengi tu
waweze kuangalia maisha yao kiutofauti na
kujibunia miradi mbalimbali ya kukizi
mahitaji yao ya kila siku na kuongezea taifa
letu kipato" alieleza @jokatemwegelo
.
.
Forbes ni jarida maarufu duniani ambalo
hufuatilia maisha ya watu maarufu duniani
na kutoa takwimu mbalimbali zikiwepo watu
wanaoingiza pesa nyingi zaidi duniani,
mastaa wanaoongoza kwa malipo ama
wajasiriamali wa kutazamiwa.

No comments

Powered by Blogger.